Sunday, November 20, 2011

Why Mt Kili lost in 7 world wonders list

Nyumba ya Tabasamu: Why Mt Kili lost in 7 world wonders list:   Mt Kilimanjaro did not make it to the final list despite a last minute surge in votes. Mount Kilimanjaro has lost the race t...

share,print,comment
WAHITIMU WA MAFUNZO YA UALIMU 2011

Mhe. Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Shukuru Kawambwa, Kwanza tunaomba kukupa pole kwa majukumu mazito uliyonayo katika ujenzi wa taifa letu. Pia tunakupongeza kwa uimara na ushupavu wako katika kusimamia masuala mbalimbali ya Elimu nchini.

Mhe. Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, lengo kuu la waraka huu kwako ni kukufikishia lalamiko letu moja kwa moja. Sisi ni wahitimu wa mafunzo ya ualimu tangu mwezi wa tano, mpaka hivi leo ni miezi zaidi ya mitano inaelekea sita bado hatujui mstakabali wetu kuhusu kupatiwa ajira. Katika shule nyingi za serikali, mambo si shwari hata kidogo. Kuna upungufu mkubwa wa walimu wenye ujuzi wa kufundisha. Ni jambo la kusikitisha kuwa walimu wenye cheti, stashahada na shahada kutoka vyuoni hawajaweza kuajiriwa. Baadhi yetu tunabangaiza ilimradi mkono uingie kinywani.

Zimetoka habari mbalimbali katika vyombo vya habari zinazoleta mkanganyiko na sisi kushindwa kuelewa mstakabali wa ajira zetu, utakuwa vipi. Kwa mujibu wa Gazeti la Mwananchi la tarehe 06 November. "NAIBU Katibu Mkuu anayeshughulikia Elimu katika Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala Za Mikoa na Serikali za Mitaa (JUMANNE SAGINI) alisema kuwa ajira tayari zimekamilika na wamepokea majina ya wahitimu 23,027 na kwamba ifikapo November 15 mwaka huu, ajira za walimu hao zitakuwa zimetangazwa. Lakini tarehe hiyo imepita na hakuna kilichotangazwa, sasa tunashindwa kuelewa, Je huyu kiongozi alidanganya umma?

Wakati hilo likiendelea Gazeti la HabariLeo la tarehe 13 November likaandika, "NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, (PHILIPO MULUGO) amesema Serikali itaajiri walimu wapya 23,000 katika kipindi cha mwaka ujao wa fedha." Sasa hapa tunachanganyikiwa, mwaka wa fedha unaanza Julai 2012. Sasa tuelewe lipi kila kiongozi anasema lake. Mhe. Waziri tunaomba utoe tamko rasmi kuhusu swala hili.

Mh. Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, tunatumaini kuwa lalamiko,kilio na ombi letu utalipokea na kulifanyia kazi. Tunakutakia afya tele na mafanikio katika shughuli mbalimbali za ujenzi wa Taifa letu na kuinua kiwango cha elimu nchini.


Ahsante sana

KAPINGAZ: BARUA YA WAZI KWA WAZIRI WA ELIMU, SERIKALI BADO I...

KAPINGAZ: BARUA YA WAZI KWA WAZIRI WA ELIMU, SERIKALI BADO I...: Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dr. Shukuru Kawambwa.  Mhe. Waziri wa Elimu na Mafunzo Ufundi, Shukuru Kawambwa, Tunaomba kwanza kuk...

share,print,comment

Monday, June 20, 2011

UTANDAWAZI NA MFUMO WA ELIMU TANZANIA

Mnamo miaka ya 1990 dunia ilishuhudia wimbi kubwa la utandwazi katika sekta mbalimbali, ikiwemo sekta ya kisiasa, kiuchumi na kijamii. Utandawazi huu ulitokana na maendeleo makubwa ya viwanda na ushindani wa kibiashara hasa katika nchi za Ulaya.
Matumizi ya teknolojia katika sehemu mbalimbali kama vile viwandani, maofisini, hospitalini, taasisi za elimu na kwingineko yalikuwa kwa kasi, ikisaidia uzalishaji na utendaji kazi kwa wingi hasa katika nchi za ulaya huku nchi za Afrika zikibaki kuangalia matokeo ya utandwazi huo kama vile mashabiki wa mpira wa miguu.
Matokeo ya uzalishajh huu yalisababisha makampuni makubwa kuongezeka na mengine kuinuka kwa kasi. Kutokana hali hiyo ikasababisha sera ya uwekezaji katika Afrika kukua na sehemu nyingine kuundwa. Nch za Afrika zililazimika kuruhusu makampuni ya kigeni kuwekeza katika nchi zao bila masharti yoyote magumu.
Watanzania tulishuhudia makampuni ya kigeni yakiingia kwa kasi nchini baada ya sera ya utandawazi kupitishwa. Pia serikali ilidiriki kuuza mashirika ya umma kwa kisingizio cha uwekezaji ili kuongeza.
Swala likaja katika kuwapatia wananchi ajira katika makampuni hayo ya wawekezaji. Kigezo kimojawapo cha kupata ajira ni ufahamu wa lugha mbalimbali. Hii ni kwa sababu wawekezaji wametoka nchi nyngi kama vile Ujerumani, Uchina, India, Uingereza, Ufaransa, Marekani n.k.Watanzania wengi tunajivunia na Kiswahili na wachache kiingereza cha kuombea maji, hii ni kutokana na mfumo mbovu wa elimu.
Mfumo wa elimu ya Tanzania haujazingatia na wala sidhani kama unampango wa kuzingatia sera ya uwekezaji ili kuweza kuwaandaa wananchi katika soko la ajira katika ulimwengu huu wa utandawazi.
Mtoto ameanza shule ya msingi darasa la kwanza mpaka la saba, lugha ya kufundishiaa ni kiswahili. Akifika shule ya upili au sekondari lugha ya kufundishia inabadilika inakuwa kingereza, kuendelea mpaka chuoni. Msingi wa huyu mtoto ambaye anaandaliwa aingie kwenye soko la ushindani wa ajira ni mbovu. Huwezi kumfananisha na mtoto wa nch kama Kenya ambaye tangia darasa la awali anatumia kiingereza pamoja na lugha nyingine za kigeni. Hivyo soko la ajira lazima litushinde.
Baada ya Rwanda na Burundi kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki, nchi ya Congo nayo iko mbioni kujiunga. Pia Sudan kusini. Lakini bado serikali inapiga porojo katika kuwaanda wananchi kuingia katika soko la ajira.
Nchi ya Rwanda imeingiza lugha mbalimbali katika mitaala yao mfano kichina. Hivyohivyo katika nchi ya Kenya.Hizi zote ni njia za kuwaandaa wananchi wao kukabiliana na ushindani wa ajira na biashara. Hapa kwetu lugha hizi zimebaki kufundishwa katika taasisi za utalii.Huku mitaala ikiboreshwa kila baada ya miaka kadhaa bila kuzingatia sera ya uwekezaji. Sasa unajiuliza wanavyokaa kuboresha mitaala hawa wanaojiita 'curriculum developers' wanaboresha nini, au wanajitengenezea mazingira ya kula posho zitokanazo na kodi za wananchi.
Bila mfumo wa elimu kubadilishwa na kuzingatia sera ya uwekezaji, wananchi wa Tanzania tutabaki kuwa walinzi katika mageti ya Wakurugenzi na Mameneja kutoka nchi za jirani.
Viongozi kazi yao ni kunenepesha matumbo yao kwa kutengeneza vikao visivyokuwa na msingi ili wapate posho zitokanazo na wavuja jasho pale Kariakoo.
Serikali kuu akiwemo Kiranja mkuu kuweni wazalendo tengenezeni mfumo wa elimu utakaotunufaisha.
Na sisi wananchi ukondoo umepitwa na wakati tuamke, tufanye mageuzi amani, amani, amani, wakati tunakufa maskini, wananeemeka wachache. Tafakari hili!.

Sunday, June 12, 2011

''23 QUESTIONS''

1. What are my streghts?
2. What specific things do i require in the job i'm seeing?
3. What are my long term goals?
4. What are my short term goals?
5. What have i already done to accomplish short term goals?
6. What do i still need to do to accomplish them?
7. What are my key values?
8. What is my personality type?
9. What do i most like doing?
10. What do i least like doing?
11. Am i a risk taker?
12. What causes me the most stress in my personal life?
13. What gives me the most pleasure in my personal life?
14. What games and sports do i enjoy,and what does that say about me?
15. Am i overly competitive?
16. Do i give up too easly?
17. Do i rise to a challenge or back away?
18. If a group of friends and acquiantances described me,what adjectives would they use?
19. What kinds of people do i enjoy working with?
20. What kind of life am i seeking?
21. What are my passions?
22. How can i make myself marketable in today's competitive job market?
23. How well do i interact with authority figures such as bosses,parents and teachers?